Wednesday, January 15, 2020

KONGAMANO LA WANAWAKE WAJASIRIAMALI MANISPAA YA SUMBAWANGA


Halmashauri ya Manispaa Sumabwanga kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii iliandaa Kongamano la Uwezeshaji Kiuchumi kwa Wanawake Wajasiriamali ndani ya Manispaa ya Sumbawanga. Kulingana na fomu ya mahudhurio Kongamano hilo lililofanyika tarehe 15/11/2019 lilihudhuriwa na Wanawake Wajasiriamali 657 sawa na 164 ya lengo la kuwafikia Wananwake 400. Mada mbalimbali ziliwasilishwa  kutoka kwa Wataalam wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Idara ya Kilimo, Idara ya Mifugo na Uvuvi, Taasisi ya PASS (Private Agricultural Sector Support) Shirika la Viwanda Vidogo la SIDO – Rukwa, TBS ofisi ya Kanda Mbeya na Benki za NMB na CRDB.

Pia katika Kongamano hilo walihudhuria Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Sumbawanga Mjini wakiongozwa na Katibu Mhe. Said King’eng’ena, pamoja naye walikuwepo Viongozi wa Jumuiya za Chama ambao walipata fursa za kutoa Salaam za Chama na kueleza shunguli na miradi ya Maendeleo inayotekelezwa Nchini na Serikali ya Awamu ya Tano.
1.0.            MADHUMUNI YA KONGAMANO
Kongamano la Uwezeshaji Kiuchumi la Wananwake Wajasiriamali lilifanyika kwa ajili ya kuamsha Ari kwa Wanawake Wajasiriamali wa Manispaa ya Sumbawanga na kuwajengea Uwezo wa Kutambua fursa mbalimbali zilizopo ndani ya Manispaa ya Sumbawanga pamoja na dhamana na nafasi yao katika Ujenzi wa Taifa.

2.0.            MALENGO MAHSUSI.
Malengo mahususi ya Kongamano la Uwezeshaji Kiuchumi la Wanawake Wajasiriamali ilikuwa ni pamoja na:- lililenga hasa katika kufikia malengo mahsusi yafuatayo:-
·         Kuwa na Kongamano la kuwakutanisha Wananwake Wajasiriamali wa Manispaa ya Sumbawanga kwa ajili ya kubadilishana uzoefu.
·         Kuwaonesha wanawake Wajasiriamali fursa zinazopatikana katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga.
·          Kutambua changamoto wanazokutana nazo na kwa pamoja kutafuta ufumbuzi wa kuzitatua changamoto hizo.
·         Kuwafanya wanawake kutambua fursa ya mikopo inayotolewa na Halmashauri kupitia 10% ya mapato ya ndani ili waweze kupata mitaji na kuanzisha na kuendeleza miradi ya kiuchumi.
·         Kuwafanya wanawake kufahamiana na kubadilishana uzoefu ili kujenga hali ya uthubutu, kujituma na kuwekeza katika Ujasiriamali.
·         Kuwaunganisha wanawake na fursa mbalimbali za Kiuchumi zinazopatikana ndani ya Manispaa ya Sumbawanga zikiwemo kilimo, ufugaji, biashara na mikopo kutoka kwenye Taasisi za Kifedha.

Mgeni rasmi katika Kongamano la Uwezeshaji Kiuchumi Wanawake Wajasiriamali wa Manispaa ya Sumbawanga Mstahiki Meya wa Manispaa Mhe. Justin Emmanuel Malisawa(Mwenye Suti ya Blue) katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali katika Kongamano la Wanawake Wajasiriamali tarehe 15 Novemba, 2019

Sehemu ya Umati mkubwa wa Wanawake Wajasiriamali waliojitokeza katika Kongamano wakisikiliza kwa makini uwasilishaji wa Mada katika Kongamano la Uwezeshaji Kiuchumi la Wanawake Wajasiriamali wa Manispaa ya Sumbawanga tarehe 15 Novemba, 2019.

Baadhi ya Watumishi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Sumbawanga wakiwa katika Picha ya Pamoja na Viongozi wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi wa Manispaa ya Sumbawanga baada ya Kongamano la tarehe 15 Novemba, 2019

Watumishi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii katika Picha ya Pamoja kuonesha ishara ya Mshikamano baada ya kuhitimisha Kongamano la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwa Wanawake Wajasiriamali wa Manispaa ya Sumbawanga tarehe 15 Novemba, 2019


Baadhi ya Watumishi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Sumbawanga na Viongozi wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi wakiwa katika picha ya pamoja kuonesha mshikamano siku ya tarehe 15 Novemba, 2019

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga Ndg. George Lupilya akitoa neno la Salaam wakati wa Kongamano la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwa Wanawake Wajasiriamali wa Manispaa ya Sumbawanga tarehe 15 Novemba, 2019